STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 20, 2011

Belle 9, Godzilla kupamba Miss Utalii Dodoma

WASANII nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini, Belle 9 na Godzilla wanatarajiwa kupamba shindano la kumsaka mrembo wa utalii wa Dodoma, Miss Utalii Dodoma litakalofanyika wiki ijayo mjini Dodoma.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamati ya Miss Utalii Tanzania kupitia Rais wake, Gideon Chipungahelo, shindano hilo litafanyika kwenye ukumbi wa Club La Aziz siku ya Oktoba 29.
Taarifa hiyo inasema, shindano hilo ambalo ni muendelezo wa kusaka wawakilishi wa mikoa kwa ajili ya fainali za taifa za kumsaka Miss Utalii Tanzania 2011-2012 litakalofanyika mapema mwakani.
Chipungahelo, alisema shindano hilo litapambwa na burudani mbalimbali ikiwemo
la wasanii wa kizazi kipya wanaotamba katika miondoko ya R&B na hip hop, Belle 9, Godzilla, na vikundi vya ngoma asilia kikiwemo Yangeyange Arts cha Dodoma.
"Shindano la Miss Utalii Dodoma, linatarajiwa kusindikizwa na burudani za wasanii Belle 9, Godzilla na vikundi vya ngoma asilia. Maandalizi kwa ujumla yapo vema kwa nia ya kulinogesha shindano hilo," Chipungahelo alisema katika taarifa hiyo.
Tayari wadhamini mbalimbali wamejitokeza kwa nia ya kulidhamini shindano hilo ambalo mbali na kusaka kisura wa mkoa, pia itatoa wawakilishi wa kushiriki shindano la taifa litakalofanyika mwakani ambalo litrahusisha washiriki toka mikoa na kanda tofauti.

Mwisho

No comments:

Post a Comment