STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 20, 2011

Filamu ya CPU kuzinduliwa rasmi Novemba 24




FILAMU mpya ya kisasa ya CPU, iliyowashirikisha wasanii nyota nchini kama Sauda Kilumanga, Dotnata Posh, Masinde, Dude na wengineo inatarajiwa kuzinduliwa rasmi Novemba 24 kwenye ukumbi wa New World Cinema, Mwenge.
Mratibu wa filamu hiyo, Evance Bukuku, alisema CPU ambayo ni kifupi cha maneno Children Protection Unity (Kitendo cha Kuwalinda Watoto), imetengenezwa na kampuni ya Haak Neel Production ikishirikisha wasanii zaidi ya 150.
Bukuku, alisema filamu hiyo iliyorekodiwa kwa teknolojia ya kisasa kwa kutumia helkopta baada ya kuzinduliwa Novemba 24, itaanza kuonyesha eneo la Mlimani City kwa muda wa wiki moja kwa kiingilio kitakachotangazwa baadae.
"Filamu yetu ya CPU ambayo imewashirikisha wahusika wakuu wanne na wasaidizi 30, itazinduliwa Novemba 24 mwaka huu kabla ya kuanza kuonyesha kwenye juumba la sinema la Mlimani City kwa wiki moja kuanzia Novemba 25- Desemba 2," alisema.
Aliongeza baada ya maonyesho hayo, kampuni yao inafanya mipango ya kwenda kuionyesha bure filamu hiyo inayozungumzia masuala mbalimbali yanayopingana na unyanyasaji na ukatili wa watoto pamoja na matendo mengine ya kihalifu.
Bukuku aliitaja mikoa itakayoenda kuonyesha filamu hiyo bure ni Mwanza, Arusha, Dodoma, Dar, Mbeya na Zanzibar.
Baadhi ya washiriki wa filamu hiyo, Steven Singh Sandhu na Sauda Kilumanga waliiambia MICHARAZO kuwa, kile ambacho watanzania walikuwa wakikisubiri kwa muda mrefu katika tasnia ya filamu sasa wamekipata kupitia filamu hiyo ya CPU.
"Ni filamu bab kubwa, ikiwa imetengenezwa kwa kiwango cha hali ya juu na ni moja ya filamu yenye uhalisi na ujumbe maridhawa kwa jamii, kitu ambacho kabla ya hapo haikuwahi kutokea," alisema Sandhu maarufu kama Salvador au .The Pride'.
Naye Sauda alisema kama mhusika mkuu katika filamu hiyo ameonyesha namna gani jamii ikishirikiana inaweza kutatua matatizo yanayowakabili watoto vikiwemo vitendo vya kikatili na uhalifu mwingine.

No comments:

Post a Comment