STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 20, 2011

Kamanda Kova kushuhudia Mbwana, Miyeyusho wakipigana Diamond Jubilee

WAKATI Mbwana Matumla 'Golden Boy' na Francis Miyeyusho 'Chichi Mawe' wakianza kutupiana 'madongo' juu ya pambano lao la kuwania mkanda wa Mabara wa UBO, Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika pambano hilo.
Mratibu wa pambano hilo la kuwania ubingwa wa Mabara wa UBO, litakalochezwa Oktoba 30, Mohammed Bawazir wa Dar World Link, alisema Kova ndiye atakayemvisha taji mshindi wa mchezo huo.
Bawazir, alisema kamanda Kova ambaye ni Mlezi wa mchezo wa ngumi nchini, amekubali mualiko wa pambano hilo litakalofanyika kwenye ukumbi wa Diamond Jubilee, Dar es Salaam.
"Maandalizi ya pambano la Mbwana Matumla atakayetetea taji lake la UBO -Inter Continental dhidi ya Francis Miyeyusho yanaendelea vema ikiwemo Kamanda Kova kukubali kuwa mgeni rasmi wa mchezo huo," alisema.
Mratibu huyo alisema kala ya wababe hao kupanda ulingoni yatafanyika mapambano mengine matano ya utangulizi likiwemo litakalowakuanisha mabondia wakike, Asha Ngedere na Salma Kiobwa.
Pambano jingine ni la kuwania ubingwa wa taifa wa PST kati ya Juma Fundi na Fadhil Majiha.
Wakati maandalizi yakiwa hivyo Mbwana na Miyeyusho kila mmoja kwa wakati wake jana amejitapa kuibuka na ushindi katika pambano hilo litakalokuwa la raundi 12 la uzani wa Bantam.
Miyeyusho alisema amejiandaa kumvua taji Matumla, licha ya kutambua ni bondia mzuri asiyetabirika.
"Niko fiti kwa ajili ya kushinda pambano hilo, sina wasiwasi, ila naomba mashabiki wake kushuhudia ninavyompiga Mbwana kwa KO," alisema.
Mbwana mwenyewe, alisema hana maneno mengi kwani anaamini yeye ndiye bingwa na haitakuwa rahisi kwake kukubali kupokwa taji lake na Miyeyusho.
"Mie sina maneno, nimezoea kutekeleza mabmbo kwa vitendo hivyo mashabiki wangu waje ukumbini kuona nitafanya nini, ila siwezi kukubali taji langu ya UBO liniondoke," alisema.
Mabondia hao watakutana katika pambano la tatu baina yao, ambapo mara mbili za mwanzo walipokutana Februari 21, 2004 na Januari 17, 2009, Mbwana aliibuka na ushindi kitu ambacho Miyeyusho amedai hakubali kupigwa tena katika mchezo huo wa Oktoba 30.

Mwisho

No comments:

Post a Comment