STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, October 20, 2011

Pambano la Maugo, Odhiambo laiva Mwanza



BONDIA mchachari wa ngumi za kulipwa nchini, Mada Maugo, amesema maandalizi ya pambano lake dhidi ya Mkenya, Joseph Odhiambo litakalofanyika keshokutwa, yamekamilika ikiwemo kutarajia kumpokea mpinzani wake kesho jijini Mwanza.
Maugo na Odhiambo wanatyarajia kuonyesha katima katika pambano lisilo la ubingwa la raundi 10 uzani wa middle, litakalosindikizwa na mabondia wakongwe nchini Joseph Marwa na Rashidi Matumla, ambalo litafanyika Jumapili uwanja wa CCM -Kirumba.
Akizungumza na MICHARAZO kwa njia ya simu toka kwenye kambi yake mjini humo, Maugo, alisema mpinzani wake anatarajia kutua jijini Mwanza kesho tayari kwa ajili ya kupima uzito siku ya Jumamosi kabla ya kupanda ulingoni Oktoba 23.
Maugo, alisema pia ameshamalizana na wasanii watakaosindikiza pambano hilo ambalo lengo lake ni kuhamasisha na kuendeleza mchezo wa ngumi katika mikoa ya Kanda ya Ziwa.
"Maandalizi ya pambano langu dhidi ya Mkenya Joseph Odhiambo yanaendelea vizuri na nawaomba mashabiki wajitokeze kwa wingi siku ya Jumapili kuweza kushuhudia mpambano huo na yale yatakayotusindikiza," alisema Maugo.
Maugo alisema miongoni mwa mapambano yatakayowasindikiza ni lile la Rashid Matumla dhidi ya Emma Kichere wa jijini Mara na Joseph Marwa atakayepigana na Chuku Dusso., huku Marwa atapigana na Chuku Duso.
"Emma Kichere ni bondia chipukizi wa mkoa wa Mara atazipiga na Matumla na Marwa atapigana na Chuku Duso anayetoka mkoa wa Mwanza, ndipo mimi na Odhiambo tutapanda ulingoni kuhitimisha michezo ya siku hiyo,' alisema Maugo.
Maugo alisema wasanii watakaosindikiza pambano lao ni H-Baba, Dudu Baya na wengine chipukizi ambao wanatokea mikoa hiyo ya Kanda ya Ziwa.
Pambano hilo la Jumapili kwa Maugo ni maalum kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa kimataifa dhidi ya Mjerumani, atayechuana nae kuwania mkanda wa IBF.

Mwisho

No comments:

Post a Comment