STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 17, 2012

Azam itafanya maajabu Afrika-Nahodha

NAHODHA wa klabu ya soka ya Azam, Aggrey Morris, amesema ana imani timu yao itafanya maajabu katika ushiriki wao wa michuano ya kimataifa. Morris, alisema japo Azam wataiwakilisha nchi kwa mara ya kwanza, bado anaamini kwa namna uongozi wao ulivyojizatiti na kujipanga tangu ilipopanda daraja, timu yao itafika kule iliposhindwa wawakilishi wengine Beki huyo wa kati anayezichezea pia timu za taifa za Zanzibar na Taifa Stars, alisema aina ya wachezaji waliopo Azam na benchi la ufundi chini ya kocha Stewart John Hall, linampa jeuri ya kuamini timu yake itatisha Afrika. "Awali ya yote tunashukuru kwa kuweza kupata nafasi hiyo ya kuiwakilisha Tanzania kwenye michuano ya kimataifa mwakani, lakini pia nataka kuwatia moyo wadau wa soka kwamba Azam haitawaangusha Afrika," alisema. Alisema, japo wachezaji karibu wote wa Azam kwa sasa wapo mapumzikoni, lakini akili zao zipo katika michuano hiyo ya Afrika. Kwa kushika nafasi ya pili katika Ligi Kuu Tanzania Bara, Azam imepata fursa ya kuiwakilisha Tanznaia katika michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika, ikiwa ni mara yao ya kwanza tangu timu hiyo ianzishwe mwaka 2004.

No comments:

Post a Comment