STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 17, 2012

Super Nywamwela sasa aibuka na Ndungwe

DANSA kiongozi wa bendi ya Extra Bongo, Hassani Mussa 'Super Nyamwela' amefyatua kibao kipya kiitwacho 'Ndungwe'akiwa katika maandalizi ya kukamilisha albamu yake ya tatu. Akizungumza na MICHARAZO, Nyamwela alisema kibao hicho kilichopo katika miondoko ya Bongofleva, amekifyatulia katika studio za AM Records chini ya prodyuza 'Maneke. Nyamwela alisema huo ni wimbo wa pili kuurekodi kwa mwaka huu baada ya awali kupakua Tumechete, alichowashirikisha 'bosi' wake, Ally Choki, Banza Stone na Athanas Montanabe. "Nimeachia wimbo mpya wa Ndungwe, nilioimba pekee yangu katika kuwaonmyesha mashabiki wangu kwamba naweza miondoko yote, kwani wimbi huu nimeutoa katika miondoko ya Bongofleva," alisema. Nyamwela alisema, kwa sasa anafanya mipango ya kurekodi video ya wimbo huo, ili mashabiki wake wapate burudani, huku akiendelea kumalizia nyimbo nyingine za kukamilisha albamu yake ya tatu binafsi. Albamu mbili za awali za bingwa huyo wa zamani wa Bolingo mkoa wa Dar es Salaam ni 'Master of the Tample' na 'Afrika Kilomondo'.
Super Nyamwela akionjesha manjonjo yake katika mazoezi ya bendi yake ya Extra Bongo

No comments:

Post a Comment