STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 17, 2012

MASKINI PATRICK MUTESA MAFISANGO!

KIFO kina usiri mkubwa na hakuna ajuae ila Mwenyezi Mungu! Ndio kauli inayoweza kuanza nayo kutokana na ukweli ni saa chache tu, tangu kiungo mahiri wa Simba, Patrick Mafisango kuitwa kwa mara ya kwanza baada ya kitambo kirefu kuwa nje ya kikosi cha timu ya taifa ya Rwanda 'Amavubi'. Mafisango aliyefariki alfajiri ya leo kwa ajali ya gari, alikuwa miongoni mwa wachezaji 32 walioitwa na kocha wa timu ya taifa ya Rwanda, Milutin 'Micho' Sredojovic kwa ajili ya kujiandaa na michuano ya kuwania Fainali za Afrika za 2013 na Kombe la Dunia za 2014. Kitambo kirefu marehemu Mafisango alikuwa hajajumuishwa katika timu hiyo kutokana na tatizo la utovu wa nidhamu, lakini kwa kiwango alichokionyesha kwa siku za karibuni akiwa na klabu ya Simba, Micho alishawishika kumuita katika timu hiyo. Hata hivyo, wakati akiwa anajiandaa kwenda Rwanda kujiunga na kambi ya timu hiyo kwa ajili ya michezo yao miwili ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya timu za Libya na Tunisia ambazo zimepangwa kucheza Mei 25 na 26. Wengine walioitwa katika kikosi hicho ni nahodha wa zamani, Hamad Ndikumana, aliyekuwa ametemwa muda mrefu, Hamdan Bariyanga, Olivier Kwizera na Francois Hakizimana na Haruna Niyonzima anayeichezea Yanga. Kwa hakika ni pigo kwa Amavubi, Simba na familia nzima ya mchezaji huyo ambaye alikuwa miongoni mwa wafungaji walioisaidia Simba kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu Tanzania Bara na kufika hatua ya 16 Bora ya Kombe la Shirikisho. Marehemu Patrick Mutesa Mafisango alizaliwa Machi 09, 1980
Innalillah Wainailahi Rajiun!

No comments:

Post a Comment