STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 17, 2012

Patrick Mutesa Mafisango afariki kwa ajali ya gari

KIUNGO mahiri wa klabu ya soka ya Simba, Patrick Mutesa Mafisango "petit' amefariki dunia alfajiri ya leo baada ya kupata ajali ya gari jijini Dar es Salaam. Kwa mujibu wa taarifa ambazo MICHARAZO imezipata na kuthibitishwa na Mwenyekiti wa klabu hiyo ya Simba, Ismail Aden Rage, Mafisango aliyekuwa mmoja wa wachezaji tegemeo wa klabu hiyo katika ushiriki wa Ligi Kuu Tanzania Bara na michuano ya Kombe la Shirikisho alifariki majira ya saa 10 akitokea klabu kujirusha. Imeelezwa kwamba, mchezaji huyo kutokla Rwanda, ingawa asili yake ni Jamhuri ya KIdeomkrasia ya Watu wa Kongo, alifariki wakati akitoka kujirusha klabu usiku na alipatwa na ajali hiyo maeneo ya TAZARA wakati akijaribu kumkwepa mwendesha Bodaboda na kujikuta wakiporomokea mtaroni na gari lake ambalo lilikuwa na watu wengine wawili. Watu hao wametajwa kuwa ni rafiki ya kiungo huyo mshambuliaji na mdogo wake ambao hata hivyo majina yake hayakuweza kupatikana mara moja. Mwenyekiti wa Simba, Ismail Rage, alisema yeye alipata taarifa na wakati akizungumza na blog hii alikuwa akiendelea kufanya mchakato wa msiba wa mchezaji wake huyo ambaye walimchukua kutoka Azam Fc. Kabla ya kutua Azam na kuonyesha uwezo mkubwa, Mafisango aliyezaliwa Machi 09, 1980 alikuwa akikipiga katika klabu ya ya nchini kwake APR ya Rwanda. Mafisango anakumbukwa kwa mchango wake mkubwa katika klabu hiyo akiifungia jumla ya mabao 11 katika Ligi Kuu Tanzania Bara msimu huu, ambapo Simba imetwaa taji ikiwapoka watani zao Yanga. Pia alikuwa mmoja wa wafungaji walioisaidia Simba kufika hatua ya 16 Bora ya Kombe la Shirikisho kabla ya kutolewa na Al Ahly Shandy ya Sudan,ambapo alikosa mkwaju wake wa penati uliosababisha Simba kung'olewa kwa jumla ya mabao 12-11. Mungu aipumzishe kwa amani roho ya marehemu Patrick Mutesa mafisango Amin!

1 comment: