STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, November 19, 2012

Choki kuwaamua Coast, Dar Modern Jumamosi


MUIMBAJI nyota na Mkurugenzi wa bendi ya Extra Bongo, Ally Choki anatarajiwa kuwa jaji katika 'pambano' la makundi mawili ya muziki wa taarab nchini, Dar Modern 'Wana wa Jiji' na Coast Modern 'Watafiti wa Mipasho litakalofanyika siku ya Jumamosi.
Mchuano wa makundi hayo yanayotamba nchini kutokana na nyimbo zao, litafanyika kwenye eneo la Kimara jijini Dar es Salaam na Choki atawaongoza majaji siku ya onyesho hilo.
Tayari makundi hayo mawili yameanza kutambiana juu ya pambano hilo ambalo litafanyika wakati kila kundi likiwa limetoka kukamilisha albamu zao mpya.
Coast linaloongozwa na mkurugenzi wake Omar Tego, limekamilisha albamu ya 'Mwanamke Kujiamini' wakati Dar Modern lililopo chini ya Mridu Ally, limefyatua albamu tatu kwa mpigo za 'Nauvua Ushoga', 'Toto la Kiafrika' na 'Ndugu wa Mume'.


No comments:

Post a Comment