STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, November 19, 2012

NTEBE AKIRI DURU LA KWANZA LILIKUWA GUMU


BEKI wa kutegemewa na timu ya soka ya Mtibwa Sugar, Salvatory Ntebe, amesema licha ya kucheza misimu kadhaa ya Ligi Kuu Tanzania Bara, hajaona ligi ngumu kama ilivyokuwa katika duru la kwanza ya msimu huu.
Aidha Ntebe aliyewahi kucheza soka la kulipwa katika klabu ya Atletico ya Burundi, alisema huenda duru la pili likawa gumu zaidi kwa vile muda wa mapumziko wa ligi hiyo timu zitakuwa zikijiimarisha maradufu.
Akizungumza na MICHARAZO juzi, beki huyo wa kati alisema duru la kwanza la ligi kuu msimu huu lilikuwa gumu na ndiop maana imekuwa na matokeo yenye kustaajabisha na timu kutoachana mbali kipointi kama msimu mingine.
"Tunashukuru kumaliza salama duru la kwanza, ila nikiri lilikuwa gumu sijawahi kuona, pale watu walipokuwa wakijua timu fulani inashinda matokeo yalikuwa kinyume na pale watu wasipotarajia kadhalika, inavutia," alisema.
Hata hivyo Ntebe alisema anadhani duru lijalo litakuwa gumu zaidi kwani timu zitatumia muda wa mapumziko kurekebisha makosa  na kuimarisha vikosi vyao, ili warejeapo duru la pili wakiwa wamejizatiti.
"Nadhani duru la pili litakuwa gumu zaidi, kila timu itatumia muda uliopo kuweka mambo sawa, hivyo kuongeza ushindani tofauti na duru lililopita lililokuwa na matokeo ya kustaajabisha karibu kila mechi," alisema.
Juu ya kikosi cha timu yake, Ntebe alisema kimepigana kadri ya uwezo wao na ndio maana kimekuwa katika nafasi iliyopo, ingawa anaamini duru lijalo timu hiyo itarejea na kasi na nguvu mpya na kufukuzana na klabu zilizopo juu.
Hadi ligi hiyo ikimaliza mzunguko wa kwanza jana kwa pambano la Ruvu Shooting na Prisons-Mbeya, Mtibwa ilikuwa nafasi ya nne na pointi 22 sawa na Coastal ila wakibebwa na uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.

Mwisho

No comments:

Post a Comment