STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, November 19, 2012

Watoto watatu wa Fella waachia mpya

Add caption



WASANII watatu chipukizi walioibuliwa na kituo cha Mkubwa na Wanae, Asnath Mathias 'Asnat', Yusuf Kondo 'K Young' na Getruda Ally 'Ge2' wameachia nyimbo zao mpya tatu tofauti, wakifuata nyayo za kaka zao kutoka kundi la TMK Wanaume Family.
Baadhi ya nyimbo za wasanii hao zimeshaanza kusambazwa katika vituo vya rdio kwa lengo la kurushwa hewani kusikika kwa mashabiki wa muziki wa kizazi kipya.
Meneja wa wasanii hao, Said Fella 'Mkubwa' aliiambia MICHARAZO kuwa, Asnat yeye amefyatua wimbo uitwao 'Tungi', wakati K Young ameachia 'Nitafika' na Ge2 akishirikiana na Abbas Maromboso amerekodi wimbo uitwao 'Nawashusha'.
Fella alisema wasanii hao ambao wanatarajiwa kutambulishwa rasmi kwa mashabiki katika onyesho litakalofanyika hivi karibuni katika klabu moja maarufu iliyopo jijini, baada ya mipango ya awali kuwatambulisha jana kushindikana.
Meneja huyo alisema chipukizi hao wameachia nyimbo hizo ikiwa ni siku chache baada ya kundi jingine analoliongoza la TMK Wanaume Family kukamilisha kibao chao kipya cha 'Mnatuonaje' alichodai ni cha kufungia mwaka 2012.
"Kituo chetu kimefanikiwa kuwafyatulia wimbo wasanii wake watatu tofauti, Asnat, K-Young na Ge2, ikiwa ni siku chache baada ya TMK Wanaume kuachia 'Mnatuonaje' wimbo unaokuja kuchukua nafasi ya ule wa 'Kichwa Kinauma'," alisema Fella.
Fella alisema kwa sasa kituo chao kinajipanga kwa ajili ya kurekodi video za nyimbo hizo ili wasanii hao chipukizi nao waanze kuuza sura wakifuata nyayo za chipukizi wenzao, Dogo Aslay, Dogo Mu, na H-Kumbi walioibuliwa na Mkubwa na Wanae.

No comments:

Post a Comment