STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, November 19, 2012

SERENGETI BOYS ILIVYOINYOA KONGO JANA KATIKA PICHA

Kipa wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17, ya Kongo Brazzaville, Ombandza Mpea Joe akilalama baada ya mpira wa adhabu uliopigwa na Mufathir Yahya Abbas kutinga nyavuni na kuwapa wenyeji ushindi wa 1-0 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam jioni ya leo.

Bao pekee leo

Kipa wa Kongo akining'inia kwenye milingoti ya lango baada ya kuukosa mpira uliopaa juu ya lango lake

Mchezaji wa Serengeti, Suleiman Hamisi Bofu akipiga mpira kichwa mbele ya beki wa Kongo, Ondongo Boungena

Beki Okombi Francis wa Kongo akiokoa mbele ya Joseph Kimwaga 

Wachezaji wa Kongo wakimdhibiti mchezaji wa Serengeti

Hussein Twaha 'Messi' akiwafunga tela wachezaji wa Kongo

Makocha wa Serengeti Jacob Michelsen na Msaidizi wake Jamhuri Kihwelo wakiwapa maelekezo vijana wao wakati mpira uliposimama kwa muda

Kipa wa Serengeti Boys, Peter Manyika akiruka hewani kupangua mchomo mkali ulioelekezwa langoni mwake 

Kipa wa Kongo, akimdondokea kiungo wa Serengeti, Farid Mussa Shah kudaka mpira, huku beki wake, Ondongo Boungena akiwa tayari kumsaidia 

Farid kulia na Ondongo kushoto

Kikosi cha vijeba wa Kongo Brazzaville

Beki Ismail Adam Gambo wa Serengeti akimdhibiti Ibara Vinny wa Kongo Brazzazille

Hussein Twaha akiwatoka wachezaji wa Kongo

Serengeti wakishangilia bao lao kwa staili ya aina yake

11 wa kwanza wa Serengeti leo

Wachezaji wa Serengeti Boys wakiimba wimbo wa taifa

Benchi la Ufundi la Serengeti Boys wakati wa wimbo wa taifa

Hussein Twaha akipasua katikati ya msitu wa wachezaji wa Kongo

Hussein Twaha akimiliki mpira mbele ya beki wa Kongo

Joseph Kimwaga akimtoka beki wa Kongo Brazzaville


Beki wa Kongo Okombi Francis baada ya kumpitia kwanja Tumaini Baraka Mosha wa Serengeti
Mudathir akiondoka na mpira

Tumaini Baraka Mosha akimtoka Okombi

Kushoto refa anasema twende, huku Tumaini Baraka Mosha akiwania mpira dhidi ya Ondongo

No comments:

Post a Comment