STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, November 19, 2012

GUINESS FOOTBALL CHALLENGE YAREJEA KWA KISHINDO



SHINDANO maarufu inalohusisha mashabiki wa soka nchini la 'Guiness Football Challenge', limerejea upya safari hii likifahamika zaidi kama 'Pan Africa Guinness Football Challenge' likishirikisha washiriki wa mataifa matano ya barani Afrika.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotumwa mwa MICHARAZO na waratibu wa shindano hilo ambalo mshidni wake atajinyakulia dola za kimarekani 900,000 litahusisha washiriki wa mataifa ya Tanzania, Kenya, Uganda, Ghana na Cameroon.
Taarifa hiyo inasema washiriki wa mataifa hayo ya Afrika Mashariki na Magharibi watachuana kuwania ubingwa wa Afrika kupitia shindano hilo maarufu la kwenye runinga.
Msimu uliopita wawakilishi waliopatikana kuiwakilisha Tanzania nchini Afrika Kusini waliweza kufanya vema, kitu ambacho wanaamini hata msimu huu wawakilioshi watakaopatikana hawataangusha watanzania katika fainali hizo.
Taarifa hiyo imeeleza usaili wa shindano la hapa nchini unatarajiwa kufanyika siku ya Jumamosi kwenye viuwanja vya Leaders na litawahusisha watu wote wenye umri kuanzia miaka 18 na wenye uwezo na ufahamu mzuri juu ya mchezo wa soka.
"Wapenzi wa soka wanakaribishwa kushiriki kwani nafasi zipo wazi kinachohitajika ni upeo wa mambo ya soka na uwezo mkubwa wa kusakata kabumbu kama vile kupiga danadana kwa manjonjo na ufundi zaidi wa kuuchezea mpira," taarifa hiyo inasema.
Katika mchakato wa kupata wawakilishi wa Tanzania katika shindano la msimu huu, kutakuwa na burudani ya kusikitiza usaili huo toka kwa wasanii mbalimbali.

Mwisho

No comments:

Post a Comment