STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, November 19, 2012

Kanumba kuenziwa kiaina Dar






ALIYEKUWA muigizaji nyota wa filamu nchini, marehemu Steven Kanumba anatarajiwa kuenziwa kiaina kupitia tamasha litakalofanyika mapema mwakani sambamba na uzinduzi wa filamu maalum juu yake iitwayo 'After Death'.
Muongozaji maarufu wa filamu nchini, mwanadada Leah Richard 'Lamata' aliiambia MICHARAZO, kuwa tamasha hilo dogo litakalooenda sambamba na uzinduzi wa filamu hiyo litafanyika Februari mwakani jijini Dar es Salaam.
Lamata, alisema katika filamu hiyo ya After Death iliyotayarishwa na Jacklyne Wolper imewashirikisha waigizaji chipukizi ambao walioibuliwa na Kanumba kupitia filamu zake kama 'This is It' na 'Uncle JJ' pamoja na msanii aliyefanana kidogo na Kanumba.
"Filamu hiyo imekamilika kwa sasa ikiwa imeshirikisha wasanii kadhaa wenye majina na wasio na majina, akiwamo mmoja aliyefanana na Kanumba, na tumepanga kufanya katamasha ka kumuenzi wakati wa uzinduzi wake," alisema Lamata.
Lamata alisema wameamua kuitengeneza filamu hiyo ya 'After Death' kama njia ya kumuenzi Kanumba kutokana na mchango wake mkubwa katika kuendeleza tasnia ya filamu na wasanii wengi kwa ujumla enzi za uhai wake.
Alisema kwa sasa wanaendelea na taratibu za kuweka  mambo sawa ili kufanikisha jambo walilokusudia, licha ya kusisitiza kua filamu hiyo mpya tayari imeshakamilika kila kitu na inasubiri kuzinduliwa na kuachiwa  mtaani.

Add caption

No comments:

Post a Comment