STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, November 19, 2012

WALIOTIMULIWA YANGA KUKIMBILIA MAHAKAMANI


UONGOZI wa klabu ya soka ya Yanga, upo hatarini kuburuzwa mahakamani na waliokuwa watendaji wa sekretarieti yao waliyoivunja hivi karibuni kwa kile kinachoelezwa kushindwa kuwalipa 'mafao' yao baada ya kuwatimua.
Yanga ilivunja sekretarierti hiyo iliyowahusisha Katibu Mkuu wake, Celestine Mwesigwa na Afisa Habari, Louis Sendeu pamoja na kamati nzima ya utendaji iliyokuwepo kwa kilichoelezwa kushindwa kufanya kazi.
Hata hivyo tangu watimuliwe Yanga, watendaji hao imeelezwa wamekuwa wakizungushwa kulipwa malimbikizo ya madeni wanayoidai Yanga na fidia ya kuvunjiwa mikataba kwa baadhi yao.
Kutokana na kuzungushwa huko kunakoelezwa inatokana na msimamo wa uongozi kutoyatambua madeni ya nyuma, watendaji hao wameanza mchakato wa kulifikisha suala lao mahakamani ili kupatiwa haki zao kisheria.
Kwa mujibu wa habari za ndani toka Yanga na kuthibitishwa na mmoja wa watendaji hao, ni kwamba tayari suala lao lipo mikononi mwa wanasheria na wakati wowote litafikishwa mahakamani.
Chnzo hicho kilisema watendaji hao watalifikisha suala hilo katika mahakama ya kazi na usuluhishi wakiamini itawasaidia kupata jasho lao.
"Ni kweli tumepanga kwenda mahakamani kwa sababu tunaona kama haki yetu inataka kupotea bure, wao ndio waliovunja mkataba vipi wasitulipe, tayari jukumu la kufungua kesi lipo mikononi mwa mwanasheria wetu," mmoja wa walalamikaji hao aliyeomba kuhifadhiwa jina lake aliiambia MICHARAZO.
Mtandao huu lilimsaka Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrance Mwalusako, ili kupata ufafanuzi wa sakata hilo la kuzungushwa kwa malipo ya watendaji hao, ambapo alisema kwa kifupi kwamba hafahamu lolote.
"Mie sijui lolote kwa sababu wakiati wakitumuliwa sikuwepo madarakani na pia sifahamu kama wanajipanga kwenda mahakamani," alisema Mwalusako.
Alipotafutwa Makamu Mwenyekiti, Clement Sanga, simu yake ilikuwa ikiita tu bila kupokelewa na hata alipotumiwa ujumbe mfupi wa maneno hakujibu chochote.
Mbali na Mwesigwa na Sendeu aliyekuwa amemaliza mkataba wake, wengine waliotimuliwa katika Sekretarieti hiyo ni Masoud Saad, aliyekuwa Ofisa Utawala na  Philip Chifuka aliyekuwa Mhasibu, huku aliyekuwa meneja wa timu, Hafidh Saleh aliyedaiwa kapangiwa majukumu mengine Yanga.

Mwisho

No comments:

Post a Comment