STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, December 31, 2012

Golden Bush, Wahenga kuuaga mwaka Tp Afrika


TIMU ya soka ya Golden Bush jioni ya leo inatarajiwa kushuka dimbani kumenyana na Wahenga Fc katika pambano maalum la kuuaga mwaka 2012 na kuukaribisha mwaka mpya wa 2013.
Pambano la timu hizo mbili zinazoundwa na wachezaji nyota wa zamani nchini, litafanyika kwenye uwanja wa TP Afrika, Sinza Dar es Salaam kuanzia majira ya jioni.
Timu hizo zitakutana katika pambano hilo huku zikiwa na kumbukumbu ya kukutana hivi karibuni kwenye dimba la uwanja huo.
Wahenga wanakumbuka kipigo cha mabao 4-2 ilichopewa na wapinzani wao siku chache baada ya kutoka sare ya bao 1-1 katika michezo iliyochezwa hivi karibuni.
Golden Bush inayomilikiwa na mmoja wa wanachama wa zamani wa Friends of Simba, Onesmo Wazir 'Ticotico', itashuka dimbani leo ikiwa na kumbukumbu ya ushindi wa mabao 3-2 iliyopata siku ya Jumamosi dhidi ya vijana nwa Chuo Kikuu.
Ticotico aliyeshindwa kuonyesha makeke yake katika pambano la Jumamosi kutokana na kuumia dakika 9 tu baada ya pambano hilo kuanza, alisema anaamini leo akijaliwa atashuka dimbani kuwaongoza wenzake kuendeleza 'dozi' yao ya mabao manne iliyokuwa inaitoa kabla ya kutibuliwa na vijana hao wa Chuo Kikuu.
"Nilikamia mechi ya Jumamosi, lakini nikashindwa kwa kuumia mapema, ila Jumatatu (leo) naweza kushuka dimbani kuwavaa wahenga," alisema Ticotico.
Katika mechi yao ya Jumamosi, Golden Bush ilipata mabao yake kupitia nyota wa zamani wa Yanga, Moro United na Prisons Mbeya, Herry Morris na Omar Msangi na inatarajiwa kushuka dimbani leo ikiwa na nyota wake kama Steven Marashi, Yahya Issa, Salum Swedi 'Kussi', Said Swedi 'Panucci', Herry Morris, Athuman Machuppa, Machotta, Majaliwa, Omar Msangi, Ticotico, Katina Shija na wakali wengine.
Wahenga wenyewe inatarajiwa kuwa chini ya nyota wa zamani wa Majimaji, Simba na Taifa Stars, Madaraka Seleman 'Mzee wa Kiminyio'.


No comments:

Post a Comment