STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, December 31, 2012

Mtanzania kuwania taji la Jumuiya ya Madola


BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa nchini, Fadhili Majia ameteuliwa na Bodi ya Wakurugenzi ya Baraza la Ngumi la Jumuiya ya Madola (CBC) kupigana na Isaac Quaye wa Ghana kuwania nafasi ya kupigana na bingwa Kevin Satchell wa Uingereza.
Mabondia hao wanatarajia kupigana katika pambano hilo la uzani wa Fly Februari 22 mwakani kwenye mji wa Accra, Ghana ambapo mshindi wa mechi hiyo ya mchujo atapata fursa ya kupigana na Satchell anayeshikilia taji hilo la Jumuiya ya Madola.
Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC) Onesmo Ngowi ambaye ni mmoja wa wakurugenzi wa CBC, alisema wajumbe wa bodi hiyo walimpigia kura Majia baada ya yeye kulipendekeza na hiyo kuibuka kidedea.
Ngowi, alisema hiyo itakuwa ni mara ya kwanaa kwa Majia kuwania mkanda huo wa Jumuiya ya Madola ambao huziunganisha nchi zote zilizotawaliwa na Uingereza.
"Bondia Mtanzania Fadhil Majia amepeta fursa ya kuteuliwa kucheza mechi ya mchujo dhidi ya Mghana, Isaac Quaye Februari 22, 2013 ili kuwania nafasi ya kupigana na bingwa wanayeshikilia taji la CBC, Kevin Satchell wa Uingereza," alisema Ngowi.
Katika hatua nyingine, Ngomi alisema CBC, imepitisha azimio la kuruhusu ubingwa wa baraza hilo katika Bara la Afrika.
Ubingwa huo utakuwa unajukikana kama 'CBC Africa Zone' na tayari wapo mabondia kadhaa wa nchi za Afrika ya Magharibi ambao wameshandaa mapambano mwakani.
"Napenda kuwahamasisha mapromota wa Tanzania kuchangamkia fursa hizi adimu na kuandaa mapambano ya ubingwa wa 'CBC Africa Zone' kwa manufaa ya mabondia wetu," alisema Ngowi ambaye pia ni Rais wa IBF Afrika/USBA.
***

No comments:

Post a Comment