STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, December 31, 2012

Majeraha yamzuia Cheka kurudiana na Mmalawi

Bondia Francis Cheka 'SMG'


BINGWA anayeshikilia mataji manne tofauti likiwemo la IBF, bondia Francis Cheka 'SMG' hataweza kupambana kwa mara nyingine tena na Mmalawi, Chiotra Chimwemwe kutokana na kuumia katika pambano lao la kwanza lililochezwa jijini Arusha wiki iliyopita.
Cheka na Chimwemwe walitarajiwa kuvaana mjini Addis Ababa, Ethiopia katika pambano maalum la kusindikiza mkutano wa Viongozi Wakuu wa nchi za Afrika, Januari 26.
Mabondia hao wangepigana kuzindikiza pambano la kimataifa kati ya Oliver McCall wa Marekani dhidi ya Sammy Retta wa Ethiopia kuwania ubingwa wa uzito wa juu IBF (IBF AMEPG).
Rais wa IBF/USBA, Onesmo Ngowi, alisema nafasi ya Cheka imechukuliwa na mkali mwingine nwa ngumi za kulipwa nchini katika uzito wa juu, Alphonce Mchumiatumbo, ingawa haijafahamika atapigana na nani.

Ngowi alisema mapambano mengine siku hiyo ya Januari 26 ni pamoja na lile la Mkenya, Daniel Wanyonyi dhidi ya Issac Hlatswayo wa Afrika Kusini watakaowania ubingwa wa IBF AMEPG uzito wa Welterweight
Pambano jingine litawakutanisha Manzur Ali wa Misri dhidi ya Harry Simon wa Namibia watakaowania taji la IBF AMEPG uzito wa Light heavyweight.

No comments:

Post a Comment