STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, December 31, 2012

Masawe Mtata ana Love position

MCHEKESHAJI mahiri wa kipindi cha 'Ze Comedy Show', Rogers Richard a.k.a. Masawe Mtata, amefyatua filamu mpya iitwayo 'Love Position', akijiandaa pia kupakua nyimbo mpya kwa ajili ya albamu yake ijayo.
Msanii huyo anayefahamika pia kwa jina la Dokta Kicheko, alisema tayari filamu hiyo ya kimapenzi ipo mtaani baada ya kuitoa wiki iliyopita akiwa ameigiza na wasanii kadhaa wenye majina na chipukizi.
Masawe Mtata, alisema filamu hiyo ya 'komedi' imekuja wakati akiwa katika harakati zake za kupakua albamu mpya ya muziki wa kizazi kipya baada ya kutamba na nyimbo kadhaa ukiwemo wa 'Siwezi Kulala'.
"Nimekamilisha na kuiachia filamu yangu mpya iitwayo 'Love Position', huku nikiwa mbioni kukamilisha albamu yangu ya tatu itakayokuwa na nyimbo nane," alisema.
Msanii huyo alisema albamu hiyo inakuja baada ya awali kutamba na albamu za 'Say Ye' au 'Unanipenda Mimi' na 'Mirinda Nyeusi' iliyofahamika pia kama 'Kicheko.com'.
Mchekeshaji huyo, alisema wakati filamu yake hiyo mpya ikiendelea kupokelewa na mashabiki wake, pia anajipanga kuandaa kazi nyingine mpya ili iwe kama 'funguo' kwa mwaka 2013 alioutabiri utakuwa na ushindani mkubwa kisanii nchini.

No comments:

Post a Comment