STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 18, 2013

AZAM WATUA SALAMA KENYA KUCHEZA KUCHEZA MECHI KESHO

Kikosi cha Azam kilipokuwa kikishangilia taji lao la Mapinduzi iliyotwaa wiki iliyopita visiwani Zanzibar kwa kuilaza Tusker ya Kenya katika mechi ya fainali.
KIKOSI cha timu ya Azam kimetua salama jijini Nairobi jana na kesho wanatarajiwa kushuka dimbani kuumana na AFC Leopard kabla ya Jumapili kuivaa Sofapaka kisha kumalizia mechi yao ya tatu dhidi ya KCB.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mtandao wa klabu hiyo ukimnukuu kocha wao mkuu, Stewart John Hall, mechi zote hizo zitachezwa kwenye uwanja wa Nyayo ambapo leo walitarajiwa kuanza mazoezi katika uwanja huo kwa ajili ya mechi hizo za kujiandaa na mechi za duru la pili la Ligi Kuu Tanzania Bara itakayoanza Januari 26.
“Tutacheza michezo mitatu, michezo yetu itahusisha timu zenye viwango vizuri katika ligi ya Kenya ambazo ni A.F.C Leopard, Sofapaka na K.C.B, mechi hizo zitasaidia kuimarisha timu yangu” alisema Stewart.
Kocha Stewart alisema watafanya mazoezi na kucheza mechi katika viwanja aina mbili vyenye nyasi za kawaida na zenye nyasi bandia kwa kuwa katika michezo ya ligi viwanja hivyo vinaendana na mazingira ya Tanzania.
Azam FC itamaliza safari yake ya maandalizi na mechi za kirafiki siku ya Jumanne kwa kuvaana naK.C.B kwenye Uwanja wa City mchezo ambao utakamilisha safari hiyo ya siku saba.
Wachezaji walioko jijini ni Mwadini Ally, Aishi Manula, Jackson Wandwi, Himid Mao, Samih Haji Nuhu, David Mwantika, Luckson Kakolaki, Jockins Atudo, Michael Bolou, Humphrey Mieno, Khamis Mcha, Gaudence Mwaikimba, Uhuru Selemani, Brain Umony, Malika Ndeule, Omary Mtaki, Abdi Kassim ‘Babi’, Abdalah Seif, Jabir Aziz, Ibrahim Mwaipopo na Salum Abubakar ‘Sure Boy’.
Father alisema kuwa mechi yao ya awali itakuwa dhidi ya Sofapaka itakayochezwa kesho kwenye dimba la Nyayo, kabla ya kucheza mechi nyingine baadae japokuwa watawakosa Gor Mahia waliokuwa wamepania kucheza nao.

No comments:

Post a Comment