STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 18, 2013

RAIS ZUMA AWAPA UBINGWA BAFANA BAFANA

Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma akionyesha ufundi wa kuchezea mpira wakati alipoitembelea timu ya taifa ya nchi hiyo, Bafana Bafana, kwenye Uwanja wa Orlando mjini Soweto, Afrika Kusini Januari 15, 2013.
Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma akipozi na wachezaji wakati alipoitembelea timu ya taifa ya nchi hiyo, Bafana Bafana, kwenye Uwanja wa Orlando mjini Soweto, Afrika Kusini Januari 15, 2013.

Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma akizungumzana wachezaji wakati alipoitembelea timu ya taifa ya nchi hiyo, Bafana Bafana, kwenye Uwanja wa Orlando mjini Soweto, Afrika Kusini Januari 15, 2013.

Kama Dinho vile... Rais wa Afrika Kusini, Jacob Zuma akionyesha ufundi wa kuchezea mpira wakati alipoitembelea timu ya taifa ya nchi hio, Bafana Bafana, kwenye Uwanja wa Orlando mjini Soweto, Afrika Kusini Januari 15, 2013.

RAIS wa Afrika Kusini, Jacob Zuma amesema anajiamini kwamba wenyeji watazima shutuma wanazoelekezewa na kubakisha nchini humo kombe la Mataifa ya Afrika 2013 kama walipolitwaa mara pekee mwaka 1996 wakati michuano ilipofanyika nchini humo.
nchini humu," alisema Rais Zuma. 
"Nilikuwa nawaeleza wachezaji kwamba (wale) wanaoshutumu hawajawahi hata kuugusa mpira. Hawaujui 'ladha' yake. 

"Tumeridhika kwamba timu imeandaliwa vyema kwa ajili ya michuano hii. 

"Ni lazima watulie, wasiwe katika presha, hawapaswi kusikiliza shutuma hizi. Ni lazima waweke akili katika kile walichojiandaa kukikafanya na watakifanya. 

"Najiamini sana wakati huu kuliko wakati mwingine wowote kwamba tutawaonyesha watu kuwa sisi ndiyo Wasauzi. 

"Nimewaambia wachezaji 'nataka kulishika kombe', na kuligusa inamaanisha kwamba tubaki nalo hapo. Na watalitwaa. Hatupaswi kuhofia chochote."

No comments:

Post a Comment