STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 18, 2013


KOCHA ZAMBIA AANZA TAMBO MAPEMA AFCON 2013

Herve Renard
Herve Renard
Herve Renard

Wachezaji wakimbeba juu kocha Herve Renard baada ya kuwaongoza kutwaa ubingwa wa Afrika mwaka jana
 


KOCHA wa timu ya taifa ya Zambia, Herve Renard anaamini kwamba timu hiyo iko vizuri zaidi ya mwaka jana, wakati wakijiandaa kutetea ubingwa wao wa Mataifa ya Afrika nchini Afrika Kusini.

Wazambia wataanza kampeni zao Jumatatu Januari 21 dhidi ya Ethiopia, wakitokea kupokea vipigo vitatu mfululizo na sare mojka katika mechi zao nne za majaribio.

Lakini Renard, ambaye aliiongoza timu hiyo kutwaa taji lao la kwanza la Afrika mwaka jana, ana furaha na maandalizi ya kikosi chake.

"Nadhani tuko vizuri kuliko mwaka jana wakati kama huu," alisema.
"Kwa wakati kama huu (mwaka jana), nilikuwa na wasiwasi mkubwa sana. Mechi zote za kujiandaa tulicheza ovyo.

"Lakini angalia kilichotokea baadaye - hatukuwa na kingine cha kuonyesha bali kombe ya ubingwa.

"Nina bahati kuwa na kikosi kama hiki."

Zambia walitoka sare ya 0-0 dhidi ya washiriki wenzao wa AFCON 2013, Morocco katika mechi ya kirafiki wiki iliyopita mjini Johannesburg, iliyofuatia vipigo vitatu mfululizo kutoka kwa Angola, Saudi Arabia na Tanzania iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Goli la pekee la mechi dhidi ya Taifa Stars ya Tanzania lilifungwa na Mrisho Ngassa.
Renard, hata hivyo, amedai kwamba matokeo hayo mabovu katika mechi za kujiandaa hayampi presha.

Kocha huyo Mfaransa amesema licha ya kwamba wao ndiyo mabingwa watetezi, nafasi kubwa ya kutwaa taji hilo wanapewa Ivory Coast na Ghana.

"Hatuwezi kusema sisi ndiyo tunaopewa nafasi. Kila mtu atakucheka ukisema hivyo. Ivory Coast na Ghana ndiyo wanaopewa nafasi."

Zambia watakabiliana na Nigeria na Burkina Faso katika Kundi C, baada ya mechi yao ya ufunguzi dhidi ya Ethiopia.

No comments:

Post a Comment