STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, January 18, 2013

Zahoro Pazi aanza kujaribiwa Bondeni, akiri kazi nzito

Zahoro Pazi (kulia) hapa akiwa mazoezi ya Azam


MSHAMBULIAJI wa Azam aliyekuwa amesajiliwa kwa mkopo na JKT Ruvu, Zahoro Pazi aliyepo nchini Afrika Kusini kuwania kucheza soka la kulipwa ameanza majaribio yake katika klabu ya Ligi Kuu ya Afrika Kusini, Bloemfotein Celtic.
Akizungumza na MICHARAZO jana usiku kutoka Afrika Kusini, Pazi alisema majaribio yake yalianza juzi katika uwanja wa klabu hiyo wa Seisa Ramabodu, uliopo mji wa Bloemfotein.
Pazi alisema mazoezi yake kwa siku ya kwanza yalikuwa ni ya mwili tu kwa ajili ya kuangaliwa stamina na pumzi na anashukuru aliyafanya mwanzo mwisho licha ya kwamba yalikuwa magumu kwake.
"Kaka nimeanza leo matizi hapa Bloemfotein but nimekutana na physic si mchezo ila nimekomaa hadi mwisho maana nilishatiwa upepo na Kilinda (kocha wa JKT Ruvu- Charles Kilinda)  hatujasuga mpira kabisa kwa leo," alisema Pazi.
Pazi aliongeza kuwa alitarajiwa kuendelea na majaribio yake leo na kuendelea kwa siku 10 kabla ya kurejea nchini kusubiri majibu yake iwapo amefuzu au la.
Mchezaji huyo aliyewahi kujaribiwa na klabu za Kaiserlauten ya Ujerumani na Nadi ya Oman, alisema anamuomba Mungu amsaidie kufuzu majaribio yake ili aweze kutimiza ndoto zake za kucheza soka la kulipwa aliloliota kwa muda mrefu.
Pazi, mtoto wa kipa wa zamani wa kimataifa wa Tanzania, Idd Pazi 'Father' aliivutia klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Afrika Kusini iliyopo nafasi ya saba katika ligi hiyo iliyosimama kupisha Michuano ya Afrika, alipokuwa DR Congo na timu yake ya Azam.
Kabla ya hapo klabu hiyo ilimuona kinda huyo katika michuano ya Kombe la Kagame iliyokuwa ikichezwa nchini na kurushwa na kituo cha Supersport cha Afrika Kusini.

No comments:

Post a Comment