STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 22, 2013

ASLAY AKIACHIA VIDEO 2, MUGOGO, DULLA YEYO WANA KIMODO



Dogo Aslay

WAKATI msanii Dogo Aslay kuiachia video za nyimbo zake mbili za 'Utachezaje' na Wahenga aliyoimba na Ally Nipishe, wakali wengine wa Kituo cha Mkubwa na Wanae, Mugogo na Duila yeyo wameana kupika wimbo wao mpya uitwao 'Kimodo'.
Meneja wa wasanii hao, Said Fella aliiambia MICHARAZO kuwa, wimbo huo mpya umefanywa chini ya prodyuza Shirko na unakuja baada ya kazi yao ya 'Wameweka' kufanya vema kwenye vituo cha radio na runinga tangu wautoe hadharani.
Fella, alisema kwa sasa wimbo huo unamaliziwa kurekodiwa kabla ya kusambazwa ili kurushwa hewani kuwapa raha mashabiki wa muziki nchini.
Aidha Fella alisema msanii Dogo Aslay ameziachia hewani video zake mbili za 'Utachezaji' na 'Wahenga' baada ya kuzisambaza wakati mkongwe Hija Cheka 'Bibi Cheka' akiendelea na mchakato wake wa kurekodi video ya wimbo wake mpya na wa tatu wa 'Nalia'.
"Bibi Cheka yeye anarekodi video ya wimbo wake wa 'Nalia' alioufanya kwa Shirko, huku Dogo Aslay akiachia video za nyimbo zake mbili za 'Utachezaje' na 'Wahenga' aliomshirikisha Ally Nipishe chini ya ufadhili wa watu wa Italia," alisema Fella.
Fella alisema wakati wasanii hao wakiendelea na michakato ya kutoa kazi zao mpya, kituo chao bado kinaendelea na utaratibu wa kuwatoa wasanii mmoja mmoja.

Mkurugenzi wa Mkubwa na Wanae, Said Fella

1 comment:

  1. Naisubiria hiyo ngoma ya Mugogo na Dula yeyo...Halafui ebu tuulizie kwa Fella, mipango yake ya Taabau imeishia wapi maana tunaona kimya au alikuwa akipima maji kwa kijiti?

    Mama Angel, Tandika

    ReplyDelete