STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 22, 2013

KUMEKUCHA MICHUANO YA NSSF





KAMATI ya usajili na uhakiki ya michuano ya Kombe la NSSF kwa vyombo vya habari jana ilianza kazi ya kuhakiki wachezaji watakaoshiriki michuano ya mwaka huu.
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Paul Urio, amesema jana jijini kuwa, kamati yao itapita kwenye vyombo vya habari 17 ambavyo timu zao zimethibitisha kushiriki michuano hiyo ili kujiridhisha juu ya uhalali wa wachezaji wao.
Alisema michuano hiyo itaanza Machi 9 katika viwanja vya TCC Sigara vilivyopo Chang'ombe jijini Dar es Salaam.
Urio alisema uhakiki huo utahusisha timu za soka kwa wanaume na netiboli kwa wanawake.
"Tunataka kujiridhisha kama wachezaji kwa kila timu waliosajiliwa ni wanahabari kweli au la," alisema Urio.
Urio aliwataja vingozi wengine wa kamati yao kuwa ni Ridhwani Ramadhani kutoka gazeti la Changamoto  ambaye pia ni katibu wao, Majuto Omary (Mwananchi), Modesti Msangi (Tumaini Media), Julius Kihampa (Jambo Leo) na Mohamed Mharizo (Mtanzania).
Hadi sasa, timu zilizothibitisha kushiriki mashindano hayo ni Tumaini, IPP, Sahara, Changamoto, Jambo Leo, Free Media na BTL.
Urio alizitaja timu nyingine kuwa ni Radio Kheri, Mlimani, TSN, TBC, New Habari, Uhuru Publishers, Habari Zanzibar, Mwananchi, Global Publishers na waandaaji NSSF





No comments:

Post a Comment