STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, February 22, 2013

Pique asononeshwa kipigo Barca



GERARD Pique alikosa furaha kutokana na kufungwa na AC Milan, lakini alikataa kujadili kiwango cha refa licha ya kosa kubwa alilofanya mwamuzi lililoizawadia Milan goli la kuongoza.
Pique alisema: "Refa anaweza kufanya makosa wakati mwingine lakini hakuna visingizio. Si refa, si uwanja, si chochote".
Beki huyo wa kati wa Barcelona alikiri kwamba "ni matokeo mabaya sana. Walipofunga goli la kwanza tukapoteza umakini. Ni lazima tuongeze ubora, tujifunze na kusubiri mechi ya marudiano Camp Nou kwa ajili ya kufuzu. Pengine sisi si wazuri kama kila mtu anavyosema".
Pique hakutaka kutoa visingizio baada ya kiwango kibovu cha timu yake na akasema: "Uwanja wa San Siro ni mgumu kuchezana tunajua kwamba Milan ni klabu kubwa. Sisi ni Barcelona na ni lazima tubadili matokeo haya".
Walioizamisha Barcelona kwenye Uwanja wa San Siro walikuwa ni Waghana watupu. Kevin Prince-Boateng na Sulley Muntari walifunga magoli magoli mawili katika ushindi wa 2-0 juzi usiku. Hiyo ilikuwa ni kwa mara ya kwanza katika historia ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, kwa wachezaji wawili kutoka nchi hiyo kufunga katika mechi moja.

No comments:

Post a Comment