STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 13, 2013

Coastal yaangukia pua Kagera, Mgambo yatakata Tanga

Hamis Shengo (kulia) wa Coastal akijaribu kumtoka Felix Themi ya Kagera Sugar katika pambano la leo. (Picha kwa hisani ya Blog ya Coastal Union)
TIMU ya Coastal Union ya Tanga jioni hii imeangukia pua baada ya kunyukwa bao 1-0 mjini Bukoba na wenyeji wa Kagera Sugar, wakati majirani zao JKT Mgambo ikinawiri nyumbani mjini Tanga kwa kuilaza JKT Oljoro kwa mabao 2-0.
Bao pekee lililowazamisha wagosi wa kaya lilitupiwa kimiani kwa kichwa na Felix Themi akitokea benchi kwenye dakika ya 58 baada ya mabeki wa Coastal kuzembea.
Kipigo hicho kinaifanya Coastal kufuata mkondo wa Mgambo ambao nao walichezea kipigo kama hicho katika mechi yao iliyopita mjini humo.
Hata hivyo Mgambo leo ilizinduka na kuzima wimbi la ushindi la JKT Oljoro kwa kuwanyuka mabao 2-0 katika pambano lililochezwa kwenye uwanja wa Mkwakwani, Tanga.
Mechi nyingine katika Ligi Kuu leo imeshuhudiwa Mtibwa ikilazimishwa sare ya 0-0 mbele ya Ruvu Shooting, huku Toto Africans wakiwa nyumbani CCM Kirumba Mwanza walilazimishwa sare ya mabao  2-2 na timu iliyozinduka tangu iwe chini ya nyota wa zamani wa Yanga, Pan na Taifa Stars, Mohammed Rishard 'Adolph' kama kocha wao, Polisi Morogoro.

No comments:

Post a Comment