STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 13, 2013

MALINZI AFUNGIWA 'VIOO' TFF BARUA YAKE YADUNDA


Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Tarehe 13 Februari 2013



Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) linapenda kuwajulisha wapenzi wa mchezo huu kuwa limepokea barua kutoka kwa Ndg. Jamal Malinzi ambayo inaomba kuangaliwa upya kwa maamuzi ya Kamati ya Rufaa za Uchaguzi ya TFF ya kuliondoa jina lake kwenye orodha ya wagombea urais wa Shirikisho.



Barua hiyo ya tarehe 13 Februari 2013 ilielekezwa kwa mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF. Baada ya kuipata barua hiyo, Sekretarieti iliwasiliana na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ambaye alielekeza kuwa Ndg. Malinzi alielekeza barua yake kwenye chombo ambacho hakikufanya uamuzi wa kuliengua jina lake na hivyo hakina mamlaka ya kuangalia upya suala hilo.



Mwenyekiti alishauri kuwa TFF imwandikie Ndg. Malinzi barua ya kumshauri kuwa aelekeze maombi yake kwenye chombo kilichofanya maamuzi kwa kuwa ndicho kinachoweza kuangalia upya maamuzi yake.



Sekretarieti pia imepokea maamuzi rasmi ya Kamati ya Rufaa za Uchaguzi ya TFF na imeshayawasilisha kwenye Kamati ya Uchaguzi ya TFF kwa ajili ya kuendelea na mchakato wa uchaguzi kwa mujibu wa Katiba na Kanuni za Uchaguzi za TFF.



Angetile Osiah

Katibu Mkuu,

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

1 comment:

  1. TFF inachokifanya sio fair kwa Malinzi, hata kama wanamtaka Nyamlani awe mrithi wa Tenga basi ingekuwa bora ashindanishwe na mgombea mwingine sio kamati ilivyofanya.
    Shabiki wa soka,
    Leila BM
    Dar

    ReplyDelete