STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 13, 2013

Yanga kuvuna nini leo kwa Lyon?

Kikosi cha Yanga kitakachovaana na African Lyon
VINARA wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga jioni ya leo wanatarajiwa kuvaana na wanaoburuza mkia katika ligi hiyo, African Lyon katika mfululizo wa mechi za duru la pili pambano litakalofanyika kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Tayari kocha msaidizi wa Yanga, Fred Minziro ameweka bayana kwamba wanaingia dimbani leo kwa lengo la kushinda mchezo huo ili kuwakimbia Azam na kujiwekea mazingira mazuri ya kutwaa taji la msimu huu.
Yanga iliyolazimishwa sare ya bao 1-1 na Mtibwa Sugar katika mechi yake ya mwisho inalingana pointi na Azam waliopo nyuma yake ambao wapo mapumzikoni wakijiandaa na mechi yao ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Kikosi cha Yanga kinakutana na Lyon ambayo imekuwa na matokeo mabaya tangu kuanza kwa duru la pili wakiwapokea Polisi Moro katika nafasi ya mkiani.
Hata hivyo Yanga isitarajie wepesi katika mechi hiyo ya leo kutokana na rekodi zilizopo pale timu hizo mbili zinapokutanana ambapo Yanga hupata tabu kuifunga timu hiyo ya Lyon.
Mbali na mechi hiyo pia leo kutakuwa na mechi nyingine kadhaa katika viwanja wa Mkwakwani Tanga, JKT Mgambo itavaana na JKT Oljoro, Coastal Union itakuwa uwanja wa Kaitaba kuumana na Kagera Sugar, huku Toto African itakuwa nyumbani kuwakaribisha Polisi Moro na Mtibwa Sugar kuivaa Ruvu Shooting.

No comments:

Post a Comment