STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 13, 2013

Juve, PSG waua Ulaya, Man U, Madrid vitani leo

Juventus stun Celtic Park thanks to Matri's early strike and temporarily silence one of the most partisan crowds in European football. The goal came following a dreadful defensive error from Efe Ambrose, who helped Nigerian win the Africa Cup of Nations just last Sunday.
Wachezaji wa Juventus wakishangilia moja ya mabao yao
WAKATI mashabiki wasoka dunia wakiwa na hamu  kushuhudia pambano kabambe kati ya Manchester United na Real Madrid, timu za Juventus na PSG usiku wa kuamkia leo wameanza vema mechi zao mtoano Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Juvetus ya Italia ikiwa ugenini nchini Scotland ilipata ushindi mnono wa mabao 3-0 dhidi ya Celtic na kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu robo fainali ya michuano hiyo.
Bao la mapema la dakika tatu toka kwa Alessandro Matri na mengine ya kipindi cha pili yaliwafanya 'kibibi' hicho cha Turin, kwenda kuisubiri Celtic katiak mechi ya marudiano ikiwa haina presha kubwa.
Mabao mengine ya Juvetus, vinara wa Ligi ya Seria A yalitupiwa kambani na Claudio Marchisio katika dakika ya 77 na Mirko Vucinic dakika saba kabla ya pambano hilo kumalizika.
Katika mechi nyingine iliyochezwa jana usiku, Valencia ya Hispania ilijikuta ikichezea kichao cha mabao 2-1 wakiwa nyumbani kutoka kwa wenyeji wao PSG ya Ufaransa.
PSG, ilijikuta hata hivyo ikimaliza pambano hilo vibaya kwa kumpoteza nyota wake Zlatan Ibrahimovic aliyelimwa kadi nyekundu dakika za lala salama.
Michuano hiyo inatarajiwa kuendelea usiku wa leo kwa mechi nyingine mbili, Manchester United ya Uingereza itasafiri mpaka Madrid, Hispania kuivaa Real Madrid katika pambano linalosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka duniani,
Pambano hilo linasubiriwa kwa hamu kutokana na hali ilizonazo timu hizo mbili ambazo zinanolewa na makocha waliowahi kuwa wapinzani wakubwa katika Ligi Kuu ya Engaland, Jose Mourinho na Sir Alex Ferguson.
Mechi nyingine inayochezwa leo itazikutanisha pia timu za Shakhtar dhidi ya Borrusia Dotmund, itakayokuwa ugenini nchini Ukraine
Utamu wa pambano hilo unachagizwa na 'vita' ya makocha waliowahi kuwa wapinzani baada ya kupewa kadi ya pili ya njano.lijikuta akimaliza mchezo huo vibaya kwa kulipwa kadi nyekundu dakika za lala salamai.

No comments:

Post a Comment