STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 13, 2013

Tegete azidi kung'ara Yanga ikiizamisha Lyon 4-0



Beki wa Yanga, David Luhende, (Kulia), akijaribu kumzuia mchezaji wa timu ya African Lyon Yusuph Mpili, wakati wa mchezo wa ligi kuu uliofanyika leo katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaa Yanga imepata ushindi wa mabao 4 -0 ikiwa imebaki kileleni



MABAO mawili ya mshambuliaji aliyerejea kwa kasi nchini, Jerry Tegete ya kipindi cha kwanza na mawili mengine ya watokea benchi Didier Kavumbagu na Nizar Khalfan katika kipindi yameipa Yanga ushindi wa mabao 4-0 mbele ya vibonde African Lyon.
Tegete aliyekuwa mwiba mkali kwa mabeki wa Lyon, alifunga mabao hayo katika pambano lililokosa msisimko kama ilivyotarajiwa lililochezwa jioni hii kwenye uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.
Ushindi huo umeifanya Yanga kuiacha Azam kwa pointi tatu katika msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara, huku Tegete akijiongezea hazina ya mabao akiwafukuzia akina Kipre Tchetche wa Azam na Didier Kavumbangu aliyefikisha bao la tisa baada ya leo kutupia moja la penati.
Yanga imefikisha jumla ya pointi 36 kutokana na michezo 16 sawa na timu nyingine 13 zinazoshiriki ligi hiyo, ikifuatiwa na Azam yenye pointi 33.
Katika pambano hilo beki wa Lyon, Mpilipili alilimwa kadi nyekudnu kwa kumchezea vibaya kiungo wa Yanga Haruna Niyonzima dakika za lala salama, huku Yanga ikikosa penati kupitia Hamis Kiiza.
Ushindi huo wa Yanga umekuja baada ya kupunguzwa kasi katika mechi iliyopita kwa kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Mtibwa Sugar na kufikisha idadi ya mechi 18 tangu timu hiyo iwe chini ya kocha Ernest Brandts

No comments:

Post a Comment