STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, February 9, 2013

Sadikina kuuza sura mara mbili



Msanii Sadikina Mussa 'Vicky'



MUIGIZAJI wa filamu anayekuja juu nchini, Sadikina Mussa 'Vicky' anatarajiwa kuuza sura katika filamu mbili tofauti za 'Hiari Yangu' na 'My Heart'.
Akizungumza na MICHARAZO, Sadikina alisema filamu hizo zilizowashirikisha wasanii mbalimbali wakiwemo nyota zimeshakamilika na zitaingizwa sokoni hivi karibuni.
Mwanadada huyo, alisema filamu zote zinahusisha masuala ya mapenzi lakini katika mitazamo tofauti na kwamba amezitendea haki kutokana na kiu aliyonayo ya kujitangaza zaidi.
Alisema katika filamu ya Hiari Yangu amecheza kama nyumba ndogo ya Kobra ambaye ndiye mhusika mkuu bila kujua kama ni mume wa shoga yake kipenzi na kuibua ugomvi uliosababisha uhasama baina yake na shogaye huyo.
"Ni moja ya kazi murua, inasisimua na ipo katika kiwango cha hali juu kama ilivyo 'My Heart'," alisema Sadikina shabiki mkubwa wa Yanga na Manchester United.


Sadikina Mussa 'Vicky'



























No comments:

Post a Comment