STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 18, 2013

Azam bwana yaani mpaka rahaaaaaa


Kikosi cha Azam

WAWAKILISHI pekee wa Tanzania, Azam imeendelea kuwapa raha watanzania baada ya jana kuwanyoa, Barracks YC  II ya Liberia kwa mabao 2-1 na kujiweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele kwenye Kombe la Shirikisho Afrika.
Katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Antonette Tubman mjini Monrovia, Liberia, Azam walienda mapumziko wakiwa nyuma kwa bao 1-0.
Bao hilo lililowashtua Azam lilifungwa dakika moja kabla ya mapumziko na Junior Barshall kabla ya Azam kuzinduka kipindi cha pili kwa kusawazisha kupitia Mkenya, Humphrey Mieno.
KInda lililosajiliwa Azam kutoka Ruvu Shooting ndiye aliyeitoa kimasomaso Azam kwa kuifungia bao la ushindi lililoifanya Azam kuwa na kazi nyepesi kwa mechi ya marudiano wiki mbili zijazo ikihitaji sare yoyote tu.
Msafara wa wawakilishi hao wa Tanzania unatarajiwa kuondoka jioni ya leo kurejea nyumbani kwa mujibu wa msemaji wa klabu hiyo, Jaffar Idd watawasilia kesho Jumanne kabla ya kuingia kambini kujiandaa na mechi zao za Ligi Kuu pamoja na pambano lake la marudiano dhidi ya Waliberia.

No comments:

Post a Comment