STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 18, 2013

Baby Madaha aja na Wither Way, aitabiria makubwa


Baby Madaha akiwa na tuzo ya AMMA

BAADA ya filamu ya 'Ray of Hope' aliyocheza kama kinara mkuu na kunyakua tuzo ya kimataifa ya AMMA, msanii Baby Madaha anatarajia kuja na filamu iitwayo 'Wither Way', ambayo ametamba itakuwa "funika bovu" kwa jinsi simulizi lake lilivyo.
Baby alisema huenda ikatikisa kuliko filamu zake nyingine alizotoa chini ya kampuni ya Pilipili kutokana na kuandaliwa katika lugha mbili tofauti, moja ikiigizwa Kiswahili na nyingine Kiingereza.
Msanii huyo alisema tayari filamu hiyo itakayoshirikisha nyota kadhaa wa fani hiyo, imeshaanza kurekodiwa na kuwataka mashabiki wake kukaa mkao wa kupata burudani.
"Nipo katika harakati za mwisho za kuibuka na filamu nyingine mpya itakayofahamika kama 'Wither Way' ambayo naamini itanipa tuzo kama nyingine nilizozicheza na kunifanya nivune tuzo nne mfululizo," alisema Baby.
Filamu za nyuma zilizompa tuzo msanii huyo ambaye pia ni mahiri katika fani ya muziki ni 'Nani' mwaka 2010, Desperado (2011) na Ray of Hope (2012) zote kupitia Tamasha la Filamu la ZIFF zikiwa kama Filamu za Mwaka kabla ya kutwaa tuzo hiyo ya AMMA nchini Nigeria.
Alisema kwa namna filamu anayokuja nayo safari hii analenga tuzo ya tamasha la maarufu la kimataifa la filamu la The Cannes.
"Sitakia kuwa mtabiri, ila lazima niseme ukweli huenda filamu ya 'Wither Way' ikabeba tuzo ya Cannes, ngoja tuone itakapotoka," alisema Baby.

No comments:

Post a Comment