STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, March 18, 2013

Mkubwa na Wanawe sasa wabeba Bendera


KUNDI la muziki wa kizazi kipya lililopo chini ya kituo cha Mkubwa na Wanawe, kinachoongozwa na Said Fella, limefyatua wimbo mpya uitwao 'Bendera' likipigwa tafu na mwalimu wao, rapa Mheshimiwa Temba.
Wimbo huo umerekodiwa katika studio za kituo hicho za Poteza Records chini ya mtayarishaji Shirko na utaanza kusambazwa kwenye vituo vya redio wiki hii.
Akizungumza na MICHARAZO, 'bosi' wa kundi hilo, Said Fella alisema wimbo huo umeimbwa na baadhi ya wasanii wa kituo hicho cha Mkubwa na Wanawe pamoja na Mheshimiwa Temba.
Aliwataja wasanii walioshiriki katika wimbo huo ambao utakuwa wa kwanza kwa kituo hicho kuimbwa na wasanii zaidi ya wawili kuwa ni Dogo Aslay, Dogo Muu, H-Kumbi, Mugogo, DY, Maromboso na Beka.
Fella alisema wakati wimbo huo ukitarajiwa kuanza kurushwa hewani, wanafanya mipango ya kutoa video yake ili mashabiki wao wapate uhondo zaidi.
"Tumeanza na audio, video ipo njiani tukiwa tumedhamiria mwaka 2013 uwe wa Mkubwa na Wanawe," alisema Fella.

No comments:

Post a Comment