STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 1, 2013

Golden Bush Veterani kuvaana na watoto wao kesho Kinesi

Kikosi cha Golden Bush kinachojiandaa na Ligi ya TFF-Kinondoni
Kikosi cha Golden Bush Veterani

BAADA ya kuikung'uta Clouds The Dream Team kwa mabao 4-1, kikosi cha Golden Bush Veterani kesho asubuhi kwenye uwanja wa Kinesi, Ubungo wanatarajia kupimana ubavu na vijana wao, Golden Bush Fc inayojiandaa na michuano ya Ligi Daraja la Nne Wilayani Kinondoni.
Golden Bush itaishiriki michuano hiyo kwa mara ya kwanza baada ya kufanikiwa kupata usajili na uongozi wake umetamba kwamba wanataka kuwa klabu ya mfano nchini kwa kupanda ngazi kutoka ligi ya TFF wilaya hadi Ligi Kuu msimu michache ijayo.
Mlezi wa timu hizo, Onesmo Waziri 'Ticotico' alisema kuwa wameandaa mechi hiyo kupima makali ya vijana wao na pambano hilo litaanza kuchezwa saa 2 asubuhi.
Ticotico alisema lengo la mechi hiyo kutoa nafasi kwa makocha wa timu ya vijana kubaini makosa ya kuyarekebisha kabla ya kuanza mbio za ligi ambayo imepangwa kuanza rasmi kesho kwa michezo kadhaa huku wao wakila shushu kwanza.
Alisema pamoja na kwamba wanacheza na vijana wao, bado watashuka dimbani kama wanacheza mechi ya fainali kwa nia ya kuhakikisha wanawapata ushindi kama walivyofanya wiki iliyopita kwa Clouds waliokuwa wakitamba kabla ya mechi yao iliyochezwa kwenye uwanja wa Tanganyika Packers, Kawe.

No comments:

Post a Comment