STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 1, 2013

Nadhipa na wenzake wa Isidingo kupanda Mlima Kilimanjaro





















WASICHANA wadogo 14 kutoka nchini Nepal, Afrika Kusini na Tanzania, akiwemo muigizaji maarufu kwenye filamu ya Isidingo wameanza safari ya kupanda mlima Kilimanjaro kupitia lango la Machame.
Kati ya wasichana hao saba wanatoka Nepal na wamewahi kupanda mlima Evarest ulioko nchini Nepal, watatu kutoka Tanzania na Balozi wa Mpango
wa Chakula Ulimwenguni (WFP) nchini Afrika Kusini, Hlubi Mboya maafuru kama Nandipa kwenye filamu ya Isidingo.
Mratibu wa WFP nchini Tanzania, Richard Regani, alisema katika nchi za Afrika na Asia, wasichana wadogo wanakutana na vikwazo vingi katika kupata elimu, ndoa za utotoni, mimba, fedha za kulipa shuleni na kazi
nyingi za nyumbani.
Alisema lengo la la safari hiyo ni  kuionyesha jamii kuwa wasichana wadogo wanaweza na wanastahili kupata huduma muhimu za kijamii bila kubaguliwa ili kuweza kujenga jamii yenye maendeleo endelevu.

No comments:

Post a Comment