STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 1, 2013

Gaucho, Uhuru waachwa msafara wa Azam


Abdulhalim Humoud 'Gaucho'

Uhuru Seleman

VIUNGO mahiri wa timu ya Azam, Abdulhalim Humoud 'Gaucho' na Uhuru Seleman ni baadhi ya nyota walioachwa kwenye msafara wa kikosi cha timu hiyo kinachotarajiwa kuondoka kesho alfajiri kwenda Sudan Kusini kurudiana na Al Nasir Juba.
Azam inatarajiwa kuvaana na Al Nasir katika mechi ya marudiano ya michuano ya Kombe la Shirikisho Afrika itakayochezwa Jumapili, huku wawakilishi hao wa Tanzania wakiwa na faida ya ushindi wa mabao 3-1 iliyopata nyumbani.
Kwa mujibu wa Katibu Msaidizi wa Azam, Twalib 'Chuma' Suleiman kikosi cha wachezaji 20 na viongozi watano na benchi zima la ufundi likiongozwa na kocha mkuu Stewart Hall watambatana pamoja katika msafara huo.Chuma aliwataja wachezaji walioambatana na timu hiyo kwa safari hiyo ya Sudan Kusini kuwa ni pamoja na makipa; Mwadini Ally na Aishi Manula, mabeki; Joackins Atudo, David Mwantika, Himid Mao, Malika Ndeule, Waziri Salum na Luckson Kakolaki.
Aliongeza wachezaji wengine ni viungo ni Kipre Balou, Jabir Aziz, Ibrahim Mwaipopo, Salum Abubakar, Humphrey Mieno, Abdi Kassim 'Babbi' na Khamis Mcha 'Vialli', huku washambuliaji wakiwa ni John Bocco 'Adebayor', Kipre Tchetche, Seif Abdallah, Brian Umony na Gaudence Mwaikimba 'Caroll'.
Baadhi ya wakali walioachwa kwenye msafara huo ni pamoja na viungo, Abdulhalim Humoud, Uhuru Suleiman Omar Mtaki, Jackson Wandiwi na Samih Haji Nuhu.
Chuma alisema kikosi chao kinaenda Sudan Kusini wakiwa na dhamira moja tu ya kuhakikisha wanapata ushindi ugenini na kusonga mbele kwenye hatua inayofuata ya michuano hiyo wanayoishiriki kwa mara ya kwanza.
Viongozi watakaoambatana na timu hiyo ni Katibu Mkuu, Nassor Idrissa, Meneja Msaidizi, Mameneja, Patrick Kahemela, Jemedari Said, Ibrahim Shikanda na Abubakar Mapwisa, huku benchi la ufundi mbali na Stewart pia wamo Kally Ongalla, Idd Abubakar Dardenne Paul na Yusuf Nzawila.

No comments:

Post a Comment