STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 1, 2013

BFT kuutangaza uchaguzi wake mkuu wiki ijayo


Katibu wa BFT, Makore Mashaga
SHIRIKISHO la Ngumi Tanzania (BTF) wiki ijayo linatarajiwa kutangaza mchakato mzima wa uchaguzi wao mkuu unaopaswa kufanyika mwaka huu kutokana muda wa uongozi wa sasa kufikia tamati mwishoni mwa mwezi huu.
Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga, alisema kwa mujibu wa Katiba iliyowaingiza madarakani miaka minne iliyopita, muda wao wa kuongoza unakoma Machi 29, hivyo wanapaswa kuitisha mchaguzi ili kupatikana kwa viongozi wapya.
Mashaga, alisema kutokana na kutambua kukaribia kumalizika kwa muda wao wa uongozi wanafanya mipango ya kuratibu mchakato mzima wa uchaguzi huo ambao watautangaza kwa wanahabari wiki ijayo.
"Ni kweli muda wetu wa kuwepo madarakani unakaribia kumalizika na tunapaswa kujipanga kuwapisha viongozi wapya, lakini hatuwezi kukurupuka hivyo mipango yote itatangazwa ndani ya wiki mbili zijazo," alisema Mashaga.
Katibu huyo alisema uongozi wao unaheshimu katiba na hivyo watahakikisha kila kitu kinaenda sawa kuhakikisha BFT inapata viongozi wengine wa kuiongoza kwa miaka mingine baada ya uongozi wao kufanya waliyoyafanya katika mchezo huo wa ngumi.
Uongozi wa sasa wa BFT uliokuwa chini ya Rais wao, Joan Minja uliingia madarakani katika uchaguzi uliofanyika Machi 14, 2009 baada ya uliokuwa uongozi wa Alhaj Shaaban Mintanga kujiuzulu kufuatia kashfa ya usafirishaji wa dawa za kulevya.

No comments:

Post a Comment