STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 1, 2013

Simba yaenda Angola na matumaini kibao

Wawakilishi wa Tanzania katika Ligi ya Mabingwa Afrika Simba


KIKOSI cha wawakilishi wa Tanzania Bara katika mashindano ya Ligi ya Klabu Bingwa Afrika, Simba wameondoka alfajiri ya leo kuelekea Angola kucheza mechi yao ya marudiano ya  michuano hiyo dhidi ya Recreativo de Libolo huku wakiahidi ushindi.

Simba imetamba kwamba licha ya kuwa nyuma kwa bao 1-0 iliyofungwa nyumbani, bado wanaamini wanaweza kurejea historia waliyowahi kuifanya mwaka 1979 na 2003 katika michuano hiyo.
Katika michuano ya mwaka 1979 Simba ililala nyumbani bao 4-0 na Mufulira Wanderers kabla ya kwenda kuwafumua wapinzani wao hao kutoka Zambia kwa mabao 5-0 na kusonga mbele.
Pia mwaka 2003 ilipata ushindi mwembamba wa bao 1-0 nyumbani dhidi ya waliokuwa mabingwa watetezi wa Afrika Zamalek na kwenda kuing'oa nyumbani kwao kwa mikwaju ya penati baada ya kulazwa 1-0 nchini Misri.
Nahodha wa Simba, Juma Kaseja alilsema jijini jana kuwa anaamini timu yao itapata ushindi ugenini kama ilivyotokea kwa wapinzani wao kupata matokeo mazuri nchini.Kaseja alisema kuwa baada ya matokeo mabaya katika mechi za ligi, wachezaji wamebadili mawazo na kuahidi kupigana katika mchezo huo wa kimataifa ili kurejesha amani ndani ya klabu yao.
"Ni mechi ngumu lakini tukumbuke Simba mara kadhaa imefanya maajabu ikiwa ugenini, tutajituma na tunaomba sala zenu ziwe pamoja nasi katika vita hii ya kusonga mbele," alisema Kaseja ambaye ndiye nyota pekee aliyebaki kwenye timu hiyo ambayo mwaka 2003 iliivua ubingwa wa Afrika, Zamalek jijini Cairo, Misri.
Kocha wa Simba, Mfaransa Patrick Liewig, naye alisema kuwa hakuna mechi rahisi na yeye alichokifanya ni kuwaandaa wachezaji wake kwa dakika 90 zilizobakia.
Liewig alieleza kuwa kufanya vibaya katika mechi za ligi kumechangia kushusha morali ya wachezaji wake lakini Jumapili watashuka dimbani wakiwa na malengo ya kusonga mbele.
Wachezaji walioondoka ni Kaseja, Abel Dhaira, Nassor Masoud "Chollo", Amir Maftah, Komalbil Keita, Juma Nyoso, Shomari Kapombe, Salim Kinje, Ramadhani Chombo 'Redondo', Amri Kiemba, Haruna Moshi 'Boban', Kiggi Makasi, Abdallah Seseme, Haruna Chanongo, Mrisho Ngassa, Felix Sunzu na Abdallah Juma huku kiongozi wa msafara akiwa ni Zacharia Hans Poppe na Muhsin Balhabou (mjumbe kamati ya utendaji wa Shirikisho la Soka Tanzania-TFF).
Mechi kati ya Simba na Libolo itachezwa Jumapili kwenye Uwanja wa Calulo uliopo katika mji wa Calulo, Angola.

No comments:

Post a Comment