STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, March 2, 2013

Real Madrid yaizima tena Barcelona

 
KIKOSI cha vijana wa Jose Mourinho 'The Only One' kimeendeleza ubabe kwa vinara wa Ligi Kuu ya Hispaniam Barcelona baada ya jioni ya leo kuitandika mabao 2-1, ikiwa ni siku chache tangu waing'oe kwenye michuano ya Kombe la Mfalme kwa kipigo cha mabao 3-1.
Bao la mapema la Karim Benzema na lile la kipindi cha pili la Sergio Ramos yalitosha kuipa Real ushindi wa pointi tatu na kujaribu kupunguza pengo la pointi dhidi ya wapinzani wao hao wa jadi wanaoongoza msimamo wakiwa mbele ya pointi 13 wakiwa na 68 dhidi ya 55 za Real kwa sasa.
'Mchawi Mweupe' Lionel Messi aliifungia Barcelona bao la kufitia machozi katika dakika ya 18 ambalo hata hivyo halikuweza kufuta uteja kwa kikosi chake kilichokuwa uwanja wa ugenini, siku chache baada ya kulala nyumbani Nou Camp.

No comments:

Post a Comment