STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 11, 2013

Golden Bush Fc haikamatiki Ligi ya TFF-Kinondoni

TIMU ya soka ya Golden Bush imezidi kuchanja mbuga kwenye Ligi Daraja la Nne wilaya ya Kinondoni, baada ya juzi kupata ushindi wa nne mfululizo  kwa kuwalaza TP Afrika kwa mabao 3-1 katika mfululizo wa ligi hiyo.
Ushindi huo wa juzi katika pambano hilo lililochezwa kwenye uwanja wa Itihad, Mwananyamala jijini Dar es Salaam limeifanya Golden Bush kuongoza msimamo wa kundi lake na kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu hatua ya pili ya michuano hiyo ninayochezwa kwenye viwanja mbaliumbali wilayani humo.
Golden Bush inayonolewa na nyota wa zamani wa soka nchini, Shija Katina na Madaraka Seleman, ilipata ushindi huo wa nne kupitia mabao yaliyofungwa na wachezaji wake nyota, Kenan Mwashinde aliyefunga mawili na Mrisho aliyefunga bao jingine.
Kabla ya ushindi huo wa juzi, Golden Bush ilianza ligi hiyo kwa kishindo kwa kuipa kipigo kitakatifu timu za Victoria ya Kijitonyama kwa kuwatandika mabao 6-1 kabla ya kuilazaa Makumbusho Talents kwa magoli 3-1 na kuizima Katabazi  na kufanya waongoze msimamo wa kundi lao wakiwa na pointi 12.

No comments:

Post a Comment