STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 11, 2013

Chelsea yafa ugenini lakini yatinga nusu fainali UEFA ndogo


Wachezaji Chelsea wakimpongeza Torres kwa kufunga bao akuongoza
LICHA ya kupokea kipigo cha mabao 3-2 kutoka kwa wenyeji wao Rubin Kazan ya Russia, Chelsea ya Uingereza imekuwa timu ya kwanza muda mfupi uliuopita kufuzu hatua ya nusu fainali ya UEFA Ndogo.
Chelsea imefanikiwa kufuzu hatua hiyo kutokana na ushindi mnono wa mabao 3-1 iliyopata katika mechi yao ya wali iliyochezwa 'darajani' mjini London hivyo kupenya kwa jumla ya mabao 5-4.
Fernando Torres aliiandikia Chelsea bao la kuongoza dakika chache baada ya kuanza kwa pambano hilo kwa kumalizia kazi nzuri ya Frank Lampard, goli lililodumu hadi wakati wa mapumziko kabla ya wenyeji kusawazisha dakika ya 51  Marcano.
Victor Moses mmopja wa wafungaji wa mabao katika pambano la wiki iliyopita baina ya timu hizo aliiongezea Chelsea bao la pili dakika nne baadaye kabla ya wenyeji kusawazisha katika dakika ya 62 kupitia kwa Gokdeniz Karadeniz kabla ya Bibras Natcho kufunga bao la ushindi kwa mkwaju wa penati dakika ya 75.
Michezo mingine ya ligi inatarajiwa kuchezwa muda mfupi ujao kwenye viwanja vingine vitatu tofauti kupata timu tatu za kuungana na Chelsea katika hatua hiyo ya nusu fainali.

No comments:

Post a Comment