STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 11, 2013

Ecuador yaingia Top 10 ya FIFA, England yaporomoka, Tanzania yapaa



NCHI ya Ecuador imeweka hostoria kwa kufanikiwa kuingia kwa mara ya kwanza kwenye Top 10 ya orodha timu bora duniani kwa mujibu wa Shirikisho la Soka Duniani, FIFA.
Kwa mujibu wa orodha iliyotangazwa na FIFA, Ecuador imeshika nafasi hiyo kutokana na ushindi wa mechi mbili mfululizo walizocheza ndani ya mwezi uliopita.
Mechi hizo ni pamoja na ile ya kirafiki ya kimataifa dhidio ya El Salvador waliposhinda mabao 5-0 na ile ya kuwania kufuzu fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Paguguay waliowalaza mabao 4-1.
Wakati Ecuador wakitinga hatua hiyo, Russia wamejikuta wakiporomoka, huku Croatia wakitinga hadi nafasi ya nne katika msimamo wa orodha hiyo mpya ya FIFA baada ya kushinda mechi zake mbili dhidi ya Wales na Serbia.
Orodha hiyo mpya ya FIFA inaoonyesha timu ya Hispania imeendelea kuongoza msimamo ikifuatiwa na Ujerumani kisha Argentina na Ureno ikikamilisha orodha ya timu Tano Bora ikitoka nafasi ya saba.
Colombia imeendelea kusalia kwenye nafasi ya sita huku England ikifuatia ikiporomoka kwa nafasi tatu, Italia imeshika nafasi ya nane baada ya kushuka kwa nafasi tatu na Uholanzi walioshuka nafasi moja wameshika nafasi ya tisa mbele ya Ecuador.
Katika orodha ya nchi za Afrika, Ivory Coast imeendelea kuongoza ikiwa ipo nafasi ya 12 duniani, ikifuatiwa na majirani zao Ghana walipo nafasi ya 22 duniani ikishika nafasi ya pili Afrika.
Zilizopo kwenye Top 10 ni Mali, Nigeria, Algeria, Tunisia, Zambia, Burkina Faso, Guinea ya Ikweta na Cameroon. Kwa ukanda wa CECAFA, Uganda imeendelea kuwa kinara ikifuatiwa na Tanzania iliyopanda kwa nafasi tatu toka 119 duniani hadi ya 116 huku Afrika ikiwa nafasi ya 33.

No comments:

Post a Comment