STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, April 11, 2013

Lyon kuendeleza maajabu leo mbele ya Azam?


Kikosi cha African Lyon

Azam Fc
TIMU ya soka ya Azam leo inatarajiwa kushuka dimbani kuvaana na African Lyon, inayopigana kuepuka kushuka daraja katika pambano pekee litakalochezwa kwenye uwanja wa Chamazi.
Lyon ambayo katika mechi yake iliyopita ilifanya maajabu kwa kuilaza Coastal Union na kuondoka mkiani, hali inayofanya mashabiki kutaka kuona kama itaendeleza ubabe huo au la.
Pambano na kwamba Lyon hiyo ni mechi yake muhimu, lakini pia kwa Azam ni muhimu zaidi katika mbio zake za kutaka kuwaengua Yanga kileleni na kuweka rekodi ya kuwa mabingwa wapya nchini.
Azam ipo nafasi ya pili nyuma ya Yanga ikiwa na pointi 43, sita zaidi ya vinara hao na iwapo itashinda itapunguza pengo hilo hadi kuwa tatu kabla ya kuvaana na Simba Jumapili uwanja wa Taifa.
Makocha wa timu hizo mbili zenye upinzani wa jadi kutoka wilaya ya Temeke, wametamba kuhakikisha wanaibuka na ushindi ili kutimiza malengo yao tofauti.
Kocha wa Azam, Muingereza Stewart Hall, alinukuliwa akisema wataingia uwanjani bila kuidharau Lyon licha ya kusaka ushindi ili kujiweka pazuri katika harakati zao za ubingwa.
Naye kocha wa Lyon, Charles Otieno, alitamba kwamba wamejipanga kushinda mchezo wa leo ili kujiweka katika nafasi nzuri zaidi ya kuepuka kurudi Ligi Daraja la Kwanza.
Kikosi cha Lyon mpaka sasa kimejikusanyia pointi 19 wakilingana na Polisi Moro wanaoshikilia mkia kwa tofauti ya uwiano wa mabao ya kufunga na kufungwa.
Ili kujua nani atakayekuwa ametimiza malengo ni kusubiri mpaka baada ya dakika 90 za pambano hilo pekee kwa siku ya leo.

No comments:

Post a Comment