STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 21, 2013

Liunda kuwatathimini waamuzi mechi ya FIFA


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhUOM9IRMZijo63-gOG0Myp2_FetrrPAa1FMIGgam1cJJeCV3Zw9RJxhccBlTqfqv1BugkRqtKZpQeEqBNDPehsoBY_0JHLwIcpdrPLMoLPcJYFT2o3h3y1-9g6SWu_adMOBBokNV6MFCU/s1600/liunda.JPG
Leslei Liunda

Na Boniface Wambura
SHIRIKISHO la Kimataifa la Mpira wa Miguu (FIFA) limemteua Leslie Liunda wa Tanzania kuwa mtathmini wa waamuzi (referee assessor) katika mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia.

Mechi hiyo ya Kundi B, Kanda ya Afrika kati ya Cape Verde na Equatorial Guinea itafanyika Juni 8 mwaka huu saa 10.30 jioni kwenye Uwanja wa Verzea mjini Praia.

Waamuzi wa mechi hiyo ambao watatoka Angola ni Martins De Carvalho Helder, Dos Santos Jerson Emiliano, Da Silva Lemos Julio na Muachihuissa Caxala Antonio. Kamishna wa mechi hiyo atakuwa Diarra Massa Momoye wa Mauritania.

No comments:

Post a Comment