STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, May 21, 2013

Wabunge nusura wachapane makofi

Wabunge Anna Kilango (kulia) na Tundu Lissu aliyeshikiliwa wakitupiana maneno

BAADA ya Bunge kuahirishwa jana, nje ya ukumbi hali haikuwa nzuri baina ya Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anne Kilango Malecela.

Mtafaruku huo uliibuka baada ya Kilango kusikika akimtuhumu Lissu kwa uchochezi, akisema kwamba amekuwa mbunge pekee anayeongoza kwa vurugu.

 
Maneno hayo hayakumfurahisha Lissu ambaye alishindwa kuvumilia na kumgeukia Kilango kwa nguvu huku baadhi ya wabunge wakishuhudia na wengine wakimzuia Lissu.
 
Hata hivyo wawili hao walimalizana kiutu uzima, japo awali ilidaiwa ilikuwa mshikemshike kama sio kuamuliwa wangeweza kuchapana makofi hadharani.

No comments:

Post a Comment