STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, May 30, 2013

Mwili wa Ngwair kuwasili nchini J'mosi, kuagwa J'2 kabla ya kuzikwa Moro J3

http://blog.greatlakesmix.com/wp-content/uploads/2013/02/ngwair-400x600.jpg
Ngwair enzi za uhai wake
MWILI wa marehemu Albert Mwangwea 'Ngwair' unatarajiwa kutua nchini siku ya Jumamosi jioni na kuagwa rasmi Jumapili kutwa nzima kabla ya kusafrishwa kwenye Morogoro kwa ajili ya mazishi yatakayofanyika Jumatatu.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Kamati ya Mazishi ya msanii huyo aliyefariki juzi nchini Afrika Kusini taratibu zote za kurejeshwa kwa mwili wa Ngwair zinaendelea vyema na kwamba kamati hiyo inaomba watu wajitokeza kuichangia kamati hiyo kutokana na ukweli kuna gharama kubwa zinazohitajika kufanikisha mambo.
Msemaji wa kamati hiyo Adam Juma, alisema mchana huu kuwa kila kitu kinaenda sawa na kwamba mwili ya marehemu Ngwair utawasili nchini jioni ya Jumamosi na Jumapili kuanzia saa 2 mpaka saa 10 wananchi watauaga mwili huo kabla ya kusafirishwa kwenda Morogoro kwa mazishi.
Juma alisema mazishi ya Ngwair yafanyika Jumatatu na kwamba kamati yao inayoongozwa na Kaka wa Marehemu Kenneth Mangwair inaratibu kila kitu kwa sasa kwa ufanisi mkubwa, ila aliwaomba mashabiki wa muziki na watanzania kwa ujumla kujitolea kwa hali na mali kuwezesha mipango ya mazishi ya Ngwair.
Mkali huyo wa miondoko ya hip hip aliyetamba na vibao mbalimbalio vikali, alifariki nchini humo alipoenda kufanya maonyesho ya muziki akiwa na msanii mwenzake, M to the P ambaye alikuwa amezimika chumbani walimokuwa wanakaa na kwa sasa inaelezwa hali yake inaendelea vyema jambo linalotoa matumaini.

No comments:

Post a Comment