STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, June 16, 2013

Kanye West, Kardashian wapata mtoto wa kike

Kardashian alipokuwa mjamzito akiwa na Kanye West

MASTAA wawili wapenzi nchini Marekani Kanye West na Kim Kardashian wamechekelea mahusiano yao kuzaa matunda baada ya wawili hao kufanikiwa kupata mtoto wa kike asubuhi ya jana.
Kardashian alijifungua mtoto huyo kwenye hospitali ya Cedars-Sinai Medical Center, Los Angeles, mtandao wa OMG umethibitisha, na ikielezwa kuwa wakati mrembo huyo alijifungua Kanye West alikuwa pembeni kushuhudia tukio hilo ambalo limekuja mwezi mmoja na tarehe ilioyotangazwa awali kwamba mtoto huyo angezaliwa Julai 11.

"Kim aliugua Ijumaa usiku na hatimaye kupata mtoto mapema jumamosi," chanzo cha hospitali kimeileza Us Weekly. “Inafurahisha, wote wako katika hali nzuri!"

Kanye West, 36, na Kim 32, huo ni uzao wao wa kwanza kwa kila mmoja ambao walianza kuwa wapenzi tangu mapema mwaka jana kabla ya Desemba, 2012 kutangaza uchumba wao kujaliwa mimba hiyo.

No comments:

Post a Comment