STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Tuesday, June 25, 2013

Wagosi wa Kaya kufanya mkutano wao Jumapili jijini Tanga

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiWU79I62KhllZ9JxAvswIJciK6IQye_4ognmhrW0xbcEP87ox-7QWFaiLuUYATuwBH3vdt9ENM0COQXx-uiT1TYgnxjKXURDOmQoHsGK2kmS72juupLW78cIsGlHOzGfd_Xpvp5jbiiZk/s320/Coastal+Union+logo.JPG

WANACHAMA wa klabu ya soka ya Coastal Union ya jijini Tanga wanatarajiwa kufanya mkutano wa pamoja ulioitishwa na uongozi wa klabu hiyo utakapofanyika siku ya Jumapili.
Kwa mujibu wa taarifa ya uongozi ilinukuliwa kwenye mtandao wa klabu hiyo ajenda kuu ya mkutano huo ni kujadili na kupanga mikakati ya ushiriki wao wa Ligi kuu Tanzania Bara inayaotarajiwa kuanza kivumbi chake Agosti mwaka huu.
Taarifa hiyto ya uongozi wa Coastal umewahimiza wanachama kujitokeza kwa wingi bila kujali wana kadi au la mradi kufanikisha mkutano huo na kujiweka mguu sawa wakiwa kitu kimoja ili kurejesha heshima iliyowapa ubingwa mwaka 1988.
Ebu jisomee mwenyewe taarifa hiyo hapo chini juu ya mkutano huo

Uongozi wa Coastal Union unawatangazia mashabiki wake walio ndani na nje ya nchi kuwa siku ya jumapili wiki hii June 30 kutakuwa na mkutano mkuu wa wanachama utakaofanyika mjini Tanga.

Mkutano huo ni muhimu kuhudhuria hata kama huna kadi ya uanachama, kwani itakuwa ni fursa pekee ya kupanga mikakati ya msimu ujao wa soka 2013/14 ili kuhakikisha kikosi imara cha wana Mangush kinaweka heshima ya soka nchini kwa kuchukua ubingwa kama walivyofanya mwaka 1988.

Uongozi unaweka wazi kuwa kwa yeyote ambaye ana malalamiko ama ushauri juu ya kuendesha timu ili kufikia mafanikio, basi ahudhurie kwenye mkutano ili kumaliza kiu yake na si kusema pembeni bila tija.

Siku hiyo mbali ya ajenda za kujenga timu pia kutakuwa na mikakati ya viongozi na kugawa majukumu kwa wanachama, pia kutajadiliwa namna ya kuhakikisha mashabiki walio mikoani na nje ya nchi wanatambulika rasmi na kukaribisha michango ya hali na mali kwa lengo moja tu, kuleta ushindi msimu ujao.

Tayari timu yetu imesharudi nyoyoni mwa wapenda soka, kilichobaki ni kuhakikisha hatuwavunji moyo wapenzi wetu cha kufanya ni kupata kadi ya uanachama ambazo zitatolewa siku hiyo, na pia kutawekwa utaratibu bora wa kuhakikisha timu inatunisha mfuko wa maendeleo.

Wanachama wengi wanawasiliana katika mitandao lakini hawajuani kwa sura hii itakuwa nafasi ya kipekee kuweza kujuana na kubadilishana mawazo, tayari wanachama wengi kutoka mikoa ya jirani wamethibitisha kuhudhuria mkutano huo, umebaki wewe tu.

Tuache kusemasema vipembeni tuelekee kwenye mkutano mkuu tarehe 30 June, 2013.

No comments:

Post a Comment